elimuyautajiiri.blogspot.com

Tuesday, March 19, 2019

SOMO LA KUMI NA NNE @elimu_ya_utajiri



Wale ambao wanamiliki biashara wanaweza kwenda mbali na biashara zao kwa muda hata wa mwaka mmoja au zaidi na watakaporudi wakakuta biashara zao zimeingiza faida zaidi na zinaenda vizuri kuliko walivyoziacha. Ila kwa mtu aliyejiajiri katika biashara yake akitoka ndani ya mwaka au zaidi, kuna asilimia kubwa kuwa hakutakuwa na biashara tena.
UTOFAUTI UKO WAPI?
Kwa kifupi tu tunaweza sema kuwa huyu aliyejiajiri anamiliki KAZI na huyu anayemiliki biashara tunasema anamiliki MFUMO WA BIASHARA na kuajiri waliobobea katika maeneo tofauti kuendesha biashara zake. Au kwa maneno mengine tunaweza sema mara nyingi huyu aliyejiajiri yeye ndio mfumo wenyewe yaani yeye ndio kila kitu na ndio maana hawezi KUONDOKA.
Tuchukue mfano mzuri wa daktari bingwa wa meno, tuseme kasoma miaka mingi tu mpaka kupata taaluma hiyo halafu akaamua kujiajiri kwa kuwa na sehemu yake ya kutoa huduma. Wewe kama mteja ukaenda kwa tatizo lako akakuhudumia vizuri sana, lazima utawatangazia marafiki na watu wengine wakikuuliza kuhusu tatizo la meno. Mara nyingi madaktari bingwa wa meno wanaweza kufanya kazi yote kuhusiana na meno wao wenyewe kwa msaada wa manesi wachache labda. Tatizo linakuja pale ambapo daktari huyo atakapoamua kwenda likizo, akienda likizo basi na kipato chake kitaenda likizo kwa maana hataingiza tena pesa mpaka pale atakaporudi.
Wamiliki wa biashara (B) wanaweza kwenda likizo maisha yao yote kwa kuwa wanamiliki MFUMO WA BIASHARA na sio KAZI. Hata B (Business owner-mmiliki wa biashara) akienda likizo pesa inaendelea kuingia. Ukitaka kufanikiwa ukiwa eneo B lazima: (1) umiliki mfumo wa biashara (2)Uwe na uwezo wa kuwaongoza wengine
Kwa wale tuliojiajiri katika biashara (S) ili kuwa wamiliki wa biashara (B) tunatakiwa tubadilike tusiwe kila kitu katika biashara zetu, kibaya zaidi wengi wetu TUNASHINDWA kufanya ivo.
#KamaUnatakaKuwaTajiriBadilishaMtazamo
#MabadilikoYanaanzaNaKujuaWapiUlipo
#MatajiriWaKesho
#MjulisheNaMwingine

No comments:

Post a Comment

Face the challenge