elimuyautajiiri.blogspot.com

Tuesday, March 19, 2019

SOMO LA KUMI NA TANO @elimu_ya_utajiri



Leo tutamalizia watu wa mwisho katika jedwali la mzunguko wa pesa wanaojulikana kama wawekezaji (Investors-I). Hawa ni watu wanaotengeneza pesa kupitia pesa, hawana haja ya kufanya kazi tena mana pesa inawafanyia kazi. Eneo I ni eneo ambalo MATAJIRI wa ukweli wanapatikana, hata kama unatengeneza pesa eneo lingine lolote (E, S, au B), kama kweli unautaka utajiri fanya hima ufike eneo I ambapo pesa itakuzalishia pesa zaidi. Fanya kazi zako za kila siku ukilenga siku moja kufika hapa. Hili ni eneo ambalo pesa inabadilika na kuwa UTAJIRI.
JEDWALI LA MZUNGUKO WA PESA
Hili limetutofautishia maeneo mbalimbali tunayozalisha pesa zetu, kwa kifupi tu:
(1) E wanapata vipato vyao kupitia ajira
(2) S wanamiliki kazi/ajira (wamejiajiri)
(3) B wanamiliki MFUMO WA BIASHARA na wana watu wanawafanyia kazi
(4) I pesa inawafanyia kazi/ wanaitumikisha pesa
Siri kubwa ya kupata utajiri ni KUTUMIA MUDA NA PESA ZA WATU WENGINE na hili linawezekana tu endapo utakuwa katika eneo B na I. Kwa kiwango kikubwa watu ambao wapo E na S ndio wale watu wengine ambao PESA NA MUDA WAO unatumika.
KWA NINI TUTOKE E  na S?
Moja ya ubaya wa kufanikiwa katika kazi uliyojiajiri (S) ni kwamba mafanikio yako yanamaanisha kufanya kazi kwa bidii zaidi na kwa muda mrefu zaidi. Tuangalie mfano wa yule daktari bingwa wa meno…kufanikiwa kwake au kuingiza kwake pesa nyingi zaidi manake awe na wateja karibu muda wote ndani ya masaa 24…yani kama ingewezekana ili ajihakikishie pesa nyingi zaidi kwa siku ahudumie hata masaa 24 YOTE Je, haya ni mafanikio ya kweli?….Na vipi kuhusu kinyozi? Mafanikio yake yakoje? Na Machinga je? Sio kwamba kila Machinga anatamani siku nzima iwe mchana? ili atengeneze pesa zaidi.....?? Ila ukiwa B mafanikio zaidi yanamaanisha nini? BIASHARA zako zimepanuka zaidi na umeajiri watu wengi zaidi wa kukufanyia kazi. Kwa maneno mengine tunasema unafanya kazi kidogo, unazalisha kingi zaidi na unapata muda mwingi zaidi wa kuwa HURU (FREE TIME)
JAMANI TUPAMBANE TUTOKE (E na S) SIKU MOJA

No comments:

Post a Comment

Face the challenge