elimuyautajiiri.blogspot.com

Monday, March 18, 2019

SOMO LA SITA @elimu_ya_utajiri



PESA ni muhimu ila kilicho muhimu zaidi ni ELIMU YA PESA. PESA huwa na tabia ya kuja na kuondoka.....ila ukiwa na elimu ya pesa utajua jinsi gani pesa inavyokwenda, utaweza kuitawala na kutengeneza utajiri. Uwezo mzuri wa kufikiri kama ambao watu wengi waliosoma au wasiosoma wanao pekee hauwezi kukusaidia kuwa TAJIRI.....hii ni kwa sababu wengi tumeenda shule lakini hatujafundishwa kuhusu kuitumikisha pesa tumefundisha kuitumikia pesa.
Elimu ya pesa itakuongoza wewe pamoja na kizazi chako kuwa MATAJIRI na kufanikiwa mazingira yoyote yale, kama uliweza kutengeneza pesa kipindi cha mh. Kikwete pia utaweza tengeneza pesa kipindi cha mh. Rais Magufuli na katika hali nyingine yoyote ile inayokuja mbeleni. Elimu ya pesa (@elimu_ya_utajiri) ipo kukupa muongozo wa kukufanya upate utajiri.
Mwalimu mzuri zaidi kuliko wote ni maisha, kuna muda yanatukaba yaani pesa ukiitafuta haipatikani, ukipata kazi mshahara unaonekana mdogo au unapata kazi inaonekana ni ngumu. Unachotakiwa ni kujua kuwa ..hayo ni mafundisho ya maisha yanayokutaka uamke kutoka kwenye usingizini. 
Kuna baadhi watakubali tu wacha maisha yaendelee kuwakaba kwa kuona hawana cha kufanya....ila wengi wetu tutapata hasira tutaamua  kupambana, lakini badala ya kupambana na maisha tutapambana na maBOSS wetu tukidai pesa tunazolipwa ni ndogo au tutapambana na kazi zetu tukidai kazi hii hailipi kabisa bora kazi fulani, na wengine huenda mbali zaidi mpaka kupambana na mume au mke. Tunasahau kwamba maisha ndo tunayotakiwa kupambana nayo.

CHUKUA SOMO HILI....Inatupasa kujilaumu sisi wenyewe kuliko kuwalaumu wengine kutokana na matatizo yetu. Kama unahisi tatizo ni mtu fulani basi fanya hima kumbadilisha ili maisha yako yabadilike, ila kama utachukulia kuwa tatizo ni lako ni rahisi kujibadilisha kuliko kumbadilisha mwingine. TUJIBADILISHE
Tunatakiwa wote kupata somo hili kwa kuwa ndilo ambalo litatupelekea kuwa wastaarabu na kuupata utajiri tunaoutaka..... la sivyo tutaishia kulaumu kazi zetu, mshahara mdogo au mabosi, huku tukiendelea kujipa matumaini kuwa kuna siku moja isiyokuwa na jina tutapata zari la pesa litakalomaliza matatizo yetu yote. 
#MjulisheNaMwingine
#MatajiriWaUkweli
#TunaMengiYaKufundishana

No comments:

Post a Comment

Face the challenge