elimuyautajiiri.blogspot.com

Monday, July 22, 2019

USIACHE KAZI

                           

HII INAMUHUSU YEYOTE AMBAE AMEAJIRIWA AU ANA NDUGU, RAFIKI YAKE AMEAJIRIWA AU ANATAFUTA AJIRA….. Hakikisha unafikisha elimu hii kwa muhusika

Moja ya tatizo kubwa sana ambalo watu wengi tunakumbana nalo leo hii ni namna gani tunaweza kuwa MATAJIRI. Na katika watu ambao wanapata ugumu zaidi katika kuwaza namna gani wanaweza kuwa MATAJIRI ni wale ambao wameajiriwa. Wengi hujiuliza waache kazi ndo waanze kuutafuta utajiri? Au wafanyaje?. Basi kama nawe ni mmoja wa wale ambao wanajiuliza hivyo @elimu_ya_utajiri inakuambia kabla hujaacha kazi jiulize maswali yafuatayo…. Je una pesa ya kuanzisha biashara? Na kama unazo… una uhakika gani hiyo biashara yako ya kwanza tu itatiki moja kwa moja? Je utakula nini ukiacha hiyo kazi?. Basi tukupe siri tu kuwa unaweza kuendelea na kazi yako na BADO UKAWA TAJIRI. Shida ambayo inawakumba waajiriwa wengi ni kwamba wanatafuta AJIRA wakilenga kupata pesa ambayo itamaliza matatizo yao yote. Kazi pekee haijawahi kumaliza tatizo la pesa…. kama unataka kuwa TAJIRI ni lazima ufanye biashara (mjasirimali) maana biashara pekee ndio ambayo haina ukomo wa mapato… unaweza ukaanza kupata mia leo mpaka kiasi chochote unachokitaka wewe siku moja kutokana na jitihada na malengo yako.

Kama unafanya kazi na bado unasumbuliwa na tatizo la kutokuwa na pesa basi mkombozi wako ni biashara na sio kutafuta kazi nyingine ya ziada. Kamwe huwezi utafuta UTAJIRI ili hali huna unachokiingiza tumboni…USIACHE KAZI. Kama unataka kuwa MJASIRIAMALI WA KWELI basi usifanye kazi kwa ajili ya pesa fanya kazi kwa ajili ya kupata maarifa fulani na uzoefu ambao utakusaidia baadae katika kuusaka utajiri wako. Fanya kazi muda ambao kazi yako inakutaka kuwa ofisini ila ukitoka kazini anza kufanya baishara yako ambayo utalenga kuikuza kila siku na kufikia kupata kipato kikubwa siku moja kuliko kile ambacho unapata kwenye mshahara wako…. KUACHA AU KUTOACHA KAZI SIKU ZA MBELENI BAADA YA BIASHARA YAKO KUANZA KUINGIZA PESA NZURI NI JUKUMU LAKO MWENYEWE. Ila kumbuka tu usifanye kazi sababu ya pesa.


Thursday, July 18, 2019

SHAUKU YA KUFANIKIWA

Kila mtu ambae anafikia umri wa kutambua dhumuni la pesa, anatamani kuwa nazo. Lakini kutamani tu hakumfanyi mtu kuwa TAJIRI. Bali SHAUKU YA KUFANIKIWA ikiambatana na nia ya dhati, kisha ikawepo mipango mikakati thabiti ya kuupata huo UTAJIRI na kuhakikisha hakuna kukata tamaa kwa lolote litakalotokea katika safari hiyo ya mafanikio basi UTAJIRI utapatikana. Anasema maneno hayo Bwana Napoleon Hill katika kitabu chake cha THINK AND GROW RICH 
Anatueleza kuwa njia ambayo SHAUKU YA KUFANIKIWA inaweza kubadilishwa na kuwa mafanikio ya kweli ambayo mtu anayataka (UTAJIRI) ina hatua SITA ambazo zinatekelezeka:
(1) Weka katika akili yako kiwango halisi cha PESA ambacho unataka kukimiliki. Usiseme pesa nyingi… Taja kiwango maalumu (Hii ina maana kubwa sana kisaikolojia, tutaelezana siku za mbeleni)
(2) Bainisha kinagaubaga namna gani utajitoa kuhakikisha unafikia malengo yako ya kumiliki hizo pesa. Mf. Kama malengo yako yatakuhitaji uwe bize walau siku nzima au  muda mwingine kuahirisha baadhi ya starehe zako basi uko tayari nk
(3)Weka muda maalumu ambao unataka kumiliki hizo pesa. Mf. Baada ya miaka mingapi? Miezi mingapi? Nk
(4)Weka mipango mikakati thabiti ambayo itakupelekea kufikia hayo malengo yako na ANZA KUTEKELEZA MARA MOJA… haijalishi uko tayari au hauko tayari kutekeleza.
(5)Andika vizuri kiasi cha pesa unachohitaji kukimiliki, muda wa mwisho ambao unatakiwa uwe umefikia lengo lako, elezea namna ambayo uko tayari kujitoa kwa ajili ya lengo lako, na elezea kwa kirefu mpango mkakati wako ambao utakupelekea  kuzipata hizo pesa. ( HAPA PANAHUSISHA KUANDIKA)
(6)Soma maelezo yako utakayoyaandika kwa sauti ya kawaida (sio kwa kunong’ona), mara mbili kwa siku, kabla hujalala usiku na unapoamka tu asubuhi. Na unaposoma…ona, hisi na kuamini kana kwamba tayari unazimiliki hizo pesa. (KUAMINI NA KUJIONA TAYARI UNAZIMILIKI HIZO PESA NI JAMBO MUHIMU ZAIDI)

USHAURI WA MTAZAMO WA KITAJIRI
Katika kufikiria kiwango cha pesa unachotaka kumiliki…..Kama UMEJIAJIRI AU UMEAJIRIWA…. Jiwekee malengo ya baada ya muda gani uwe una MZUNGUKO WA PESA UNAOUHITAJI (CASH FLOW) kwa mwezi kutoka vyanzo vyako mbalimbali ambavyo unataka kuvimiliki na ambavyo vitaingiza hiyo PESA bila uwepo wako kabisa au ushiriki wako mdogo. Mfano, unaweza sema baada ya miaka mitano nitataka niwe na MZUNGUKO WA PESA wa sh. LAKI TATU bila mimi kuwepo kwenye vyanzo hivyo halafu weka mikakati na kuanza kuitekeleza. Hii itawasaidia WAAJIRIWA na WALIOJIAJIRI kufikia UTAJIRI wa kweli siku moja na sio tu kutegemea mshahara maisha yote. SAFARI NJEMA KWAKO AMBAE UTATEKELEZA…..



Thursday, May 9, 2019

SOMO LA AROBAINI



Watu wengi wanaamini kutengeneza pesa nyingi zaidi kutatatua matatizo yao yote ya pesa. Ila mara nyingi husababisha matatizo makubwa zaidi. Moja ya sababu kubwa inayosababisha matatizo mengi ya pesa kwa watu ni kwamba hawajawahi kufundishwa jinsi ya kudhibiti mzunguko wao wa pesa. Wamefundishwa kujua kusoma, kuandika, kuendesha gari nk lakini sio namna ya kudhibiti mzunguko wao wa pesa. Bila ya kulijua hili wanaishia kuwa na matatizo ya pesa kila kukicha na kuendelea kufanya kazi kwa bidii zaidi wakiamini kwamba kutengeneza pesa nyingi zaidi kutamaliza matatizo yao. JUA KWAMBA PESA NYINGI HAZITAMALIZA MATATIZO YAKO YA PESA KAMA UKISHINDWA KUDHIBITI MZUNGUKO WAKO WA PESA. Pesa nyingi zaidi huwafanya watu wengi kuwa maskini kwa sababu huongeza matumizi na kuangukia kwenye madeni makubwa kila mara wanapoongezwa mshahara.
Unatakiwa ukae chini uweke mpango wa kudhibiti matumizi na kupunguza madeni hali kadhalika kupunguza vitu ambavyo vinakupunguzia pesa mfukoni. Nimekuandalia hapa chini namna ambayo itakuwezesha kudhibiti mzunguko wako wa pesa.
Ila fanya hivi kabla sijakuambia:
(1) Ainisha kipato chako na matumizi yako kwa mwezi.
(2) Angalia eneo ambalo unazalisha kipato chako (mwajiriwa, umejiajiri, mmiliki wa biashara au mwekezaji)------Kumbuka mmiliki wa biashara ni yule ambaye anaweza akaondoka mbali na biashara yake hata mwaka au miaka miwili lakini akakuta biashara yake bado ipo au imekuwa zaidi. Ukiona huwezi kufanya hivyo basi jua umejipa kazi mwenyewe/ umejiajiri
(3) Ainisha eneo gani ambalo unataka kuzalisha pesa nyingi zaid baada ya miaka mitano (Baada ya miaka mitano unataka kuzalisha pesa nyingi kama mwajiriwa, aliyejiajiajiri, mmiliki wa biashara au mwekezaji?)
Haya sasa baada ya kufanya hivyo uko tayari kuanza mpango mkakati wa kudhibiti mzunguko wa pesa. Ni hatua mbili tu za kuzifanya:
(1) Jilipe mwenyewe kwanza 

Tenga asilimia fulani kila unapopata kipato au mshahara wako kwa ajili ya kuwekeza. Na ukikitunza usikitoe ulipokitunza mf. Benki mpaka pale utakapoona kuwa uko tayari kuwekeza.

(2) Lipa deni

Kama una madeni basi tenga asilimia nyingine kwa ajili ya kulipa deni mpaka libakie sifuri na uongeze hiyo asilimia uliyoweka kulipa deni lako la mwisho kwa ajili ya kuwekeza. Na hakikisha kipindi unalipa deni usiongeze deni lingine.


Wednesday, May 8, 2019

MUNGU NA UWEKEZAJI (SOMO LA 1)


 SOMO  JIPYA LA ELIMU YA UTAJIRI 

KUHUSU MUNGU NA UWEKEZAJI

NA MADAM FAITH

KARIBU SANA 




Face the challenge