
HII INAMUHUSU YEYOTE AMBAE AMEAJIRIWA AU ANA NDUGU,
RAFIKI YAKE AMEAJIRIWA AU ANATAFUTA AJIRA….. Hakikisha unafikisha elimu hii kwa
muhusika
Moja ya tatizo kubwa sana ambalo watu wengi
tunakumbana nalo leo hii ni namna gani tunaweza kuwa MATAJIRI. Na katika watu ambao
wanapata ugumu zaidi katika kuwaza namna gani wanaweza kuwa MATAJIRI ni wale
ambao wameajiriwa. Wengi hujiuliza waache kazi ndo waanze kuutafuta utajiri? Au
wafanyaje?. Basi kama nawe ni mmoja wa wale ambao wanajiuliza hivyo @elimu_ya_utajiri
inakuambia kabla hujaacha kazi jiulize maswali yafuatayo…. Je una pesa ya
kuanzisha biashara? Na kama unazo… una uhakika gani hiyo biashara yako ya
kwanza tu itatiki moja kwa moja? Je utakula nini ukiacha hiyo kazi?. Basi
tukupe siri tu kuwa unaweza kuendelea na kazi yako na BADO UKAWA TAJIRI. Shida
ambayo inawakumba waajiriwa wengi ni kwamba wanatafuta AJIRA wakilenga kupata
pesa ambayo itamaliza matatizo yao yote. Kazi pekee haijawahi kumaliza tatizo
la pesa…. kama unataka kuwa TAJIRI ni lazima ufanye biashara (mjasirimali)
maana biashara pekee ndio ambayo haina ukomo wa mapato… unaweza ukaanza kupata
mia leo mpaka kiasi chochote unachokitaka wewe siku moja kutokana na jitihada na
malengo yako.
Kama unafanya kazi na bado unasumbuliwa na tatizo la
kutokuwa na pesa basi mkombozi wako ni biashara na sio kutafuta kazi nyingine
ya ziada. Kamwe huwezi utafuta UTAJIRI ili hali huna unachokiingiza tumboni…USIACHE
KAZI. Kama unataka kuwa MJASIRIAMALI WA KWELI basi usifanye kazi kwa ajili ya
pesa fanya kazi kwa ajili ya kupata maarifa fulani na uzoefu ambao utakusaidia
baadae katika kuusaka utajiri wako. Fanya kazi muda ambao kazi yako inakutaka
kuwa ofisini ila ukitoka kazini anza kufanya baishara yako ambayo utalenga
kuikuza kila siku na kufikia kupata kipato kikubwa siku moja kuliko kile
ambacho unapata kwenye mshahara wako…. KUACHA AU KUTOACHA KAZI SIKU ZA MBELENI
BAADA YA BIASHARA YAKO KUANZA KUINGIZA PESA NZURI NI JUKUMU LAKO MWENYEWE. Ila
kumbuka tu usifanye kazi sababu ya pesa.
