elimuyautajiiri.blogspot.com

Saturday, March 30, 2019

SOMO LA ISHIRINI NA TANO @elimuyautajiri



Bwana Robert Kiyosaki amegawanya wawekezaji katika madaraja/aina tano: (1) Ambao HAWANA KABISA CHA KUWEKEZA
Pia daraja hili linahusisha baadhi ya wanaotengeneza pesa nyingi. (2) WATUNZAJI WA PESA (wale wa kusevu—savers)
Wale wa kuweka pesa benki, kwenye vibubu, wanaosubiria kupata viinua mgongo wakistaafu n.k (3) Ambao WAKO BIZE SANA. 
Hawa ni wale ambao kazi ya kuwekeza wamewaachia wengine kwa kuwa wako bize sana kiasi cha kushindwa kujifunza uwekezaji. (4) Ambao WANAONA WANAWEZA  KUFANYA KILA KITU WENYEWE.
Wengi ya waliostaafu wanaingia katika aina hii ya wawekezaji (5) WAMILIKI WA BIASHARA WALIOAMUA KUWEKEZA
Tukikumbushana kuwa hawa sio waliojiajiri katika biashara zao bali wanaomiliki biashara (B) wakaamua kuwekeza (I). Na hapa ndipo ambapo tunashauriwa kulenga kama tunawaza kuwa WAWEKEZAJI siku moja.

Tuendelee kuwa pamoja tutakuchambulia kwa kirefu kila daraja la wawekezaji.
#MjulisheNaMwingineAfaidike

Attachments area

No comments:

Post a Comment

Face the challenge