elimuyautajiiri.blogspot.com

Wednesday, April 24, 2019

SOMO LA THELATHINI NA TATU


Kwa wale waliojitathmini  na kujiona kuwa wapo daraja la kwanza.
Kama hauna kitu chochote kinachokuingizia pesa na una vitu vingi vinavyokutolea pesa mfukoni basi wewe unaanzia katika daraja la chini kabisa yaani unaanza SIFURI. Na kama una madeni mengi basi uwekezaji wako mkubwa utakuwa ni kuondokana na hayo madeni. Hakuna ubaya kwa mtu kuwa na madeni labda kama haufanyi jitihada zozote. Unaweza kupoteza biashara na kuwa katika madeni makubwa na ikakuchukua muda kuondokana na madeni hayo mpaka kufikia sifuri yaani haudaiwi na mtu.
Kitu unachotakiwa kufahamu ni kwamba unatakiwa ujifunze kutokana na makosa na ukubali kukabiliana na lolote litakalotokea kutokana na makosa yako utakayoyafanya au uliyoyafanya na HILI NI FUNZO KUBWA UNALOTAKIWA KUFAHAMU KATIKA MAISHA YAKO YA KILA SIKU. Usipojifunza kutokana na makosa yako kamwe hautakuwa pale unapotaka kuwa siku moja.
Tutapeana mwongozo siku za usoni namna ambayo itakusaidia kuondokana na MADENI.
Usisahau kutembelea
elimuyautajiri.blogspot.com
Attachments area

No comments:

Post a Comment

Face the challenge