Kama wewe ni mtunzaji wa pesa mzoefu (msevuji) kuwa makini sana hasa kama wewe unatunza pesa benki, kwenye kibubu au katika ule mpango wa kusubiria uipate pesa yako utakapostaafu.
Kutunza pesa ni njia ya watu ambao hawataki kujifunza chochote kwani haihitaji maarifa yoyote ya pesa ili uweze kutunza pesa zako. Inasemekana unaweza mfundisha nyani kutunza pesa na akawa anatunza. Ubaya wa kutunza pesa ni kwamba unachojifunza ni kidogo sana na endapo pesa yako itateketea kwa namna yoyote ile utajikuta hauna pesa pia hakuna ulichojifunza chochote.
Kama wewe ni mtunzaji mzuri sana wa pesa basi unashauriwa kutafuta kozi zozote (elimu yoyote ya jambo fulani) zinazohusiana na uwekezaji na kuangalia kitu gani kitakuvutia halafu ukifanye. Kama hakuna kinachokuvutia kuwekeza basi endelea kutunza pesa zako.
Kuna msemo wa kizungu unasema "In General, SAVERS ARE LOSERS" naomba mnisaidie tafsiri hapa chini.... Usisahau kutembelea

No comments:
Post a Comment