elimuyautajiiri.blogspot.com

Wednesday, April 24, 2019

SOMO LA THELATHINI NA TANO


Kama hutaki kumkabidhi mtu pesa yako akuwekezee basi utakuwa unataka kupata elimu na kuweza kuzisimamia pesa zako wewe mwenyewe. Ukiona ivo jua unafaa kuwa mwekezaji namba 4 kuliko yule namba 3 anayemkabidhi mtu mwingine majukumu ya uwekezaji.... Na Kama unatufatilia hapa ukiwa  mwekezaji aliyebobea katika jambo fulani mf. masuala ya fenicha, makapeti, elimu n.k basi HONGERA SANA. Ni watu wachache sana wanaoamua kuwekeza muda wao katika kujifunza na kuweza kuzisimamia pesa zao.
Ili uweze kufanikiwa kama mwekezaji namba 4 (wawekezaji waliobobea katika jambo fulani n.k) ni kuendelea kujifunza, kuwa na walimu wazuri (watu waliokutangulia katika jambo hilo wakafanikiwa) bila kusahau marafiki ambao mnaendana fikra.
Wawekezaji namba 4  wanayaendesha maisha yao wakijua kwamba makosa yao ni nafasi kwao kujifunza na kukua zaidi na si vinginevyo. Hofu ya kuwekeza haiwatishi zaidi ya kuwapa MOTISHA.
Usisahau kutembelea 

elimuyautajiri. blogspot.com

No comments:

Post a Comment

Face the challenge