elimuyautajiiri.blogspot.com

Tuesday, March 19, 2019

SOMO LA ISHIRINI NA MOJA @elimu_ya_utajiri



Tuanze kwa kuangalia mfano hai ambao unaweza tokea au hutokea katika maisha yetu ya kawaida. Tuseme leo kampuni unayoifanyia kazi inauzwa na boss anaekuja ni mpya. Kiuhalisia sio kwamba wote mliokuwa mnafanya kazi chini ya boss wa mwanzoni mtaendelea kuwa na kazi baada ya kuingia bosi mwingine.Wengi tutaishia kulia machozi ya damu kwa kuwa kukosa kazi kwa wengi wetu kunamaanisha maisha yatakuwa magumu. Unajua kwa nini wengi tutalia? Hii ni kwa sababu wengi tuliwaza kufanikiwa kutokana na mshahara au tunaweza sema tulikuwa tunategemea mshahara utufanye kuwa MATAJIRI siku moja…hii ina maanisha kwamba ulikuwa unamtegemea boss wako akufanye uwe TAJIRI..wengi tunasahau kuwa jukumu la boss ni kutupa MSHAHARA tu …ila kama unataka kuwa TAJIRI ni jukumu lako wewe mwenyewe na hili huanza pale tu unapoanza kupokea MSHAHARA.
Kama hauna maarifa  ya kutosha katika kuzitawala pesa zako, pesa za kiwango chochote hazitakunusuru na janga la umaskini. Kama utabajeti pesa yako vizuri na kupata maarifa ya kumiliki biashara kubwa kubwa au uwekezaji basi utakuwa upo katika njia ya kuwa TAJIRI.Tunatakiwa kufahamu  tofauti kubwa iliyokuwepo kati ya TAJIRI na maskini  ni jinsi wanavyotumia muda wao  ambao wanakuwa huru (FREE). Wengi tuko bize tukihangaika na mshahara tukasahau kujenga kesho yetu, kama utakuwa bize na mshahara basi utakuwa bize maishani. Ila kama unataka kuwa bize basi ni bora ukawa bize kwa yote mawili yaani mshahara au kujiajiri na kuhangaika kuwa na biashara kubwa au kuwekeza. 

Ila tunashauriwa kabla hatujawa wawekezaji inabidi tuanze kuhangaika kumiliki biashara kubwa kubwa/ kupanua biashara. Kwa nini? Hii ni kwa sababu ya kujipa muda wa kutosha kupata UZOEFU NA ELIMU hali kadhalika KUHAKIKISHA TUNAKUA NA MZUNGUKO MZURI WA PESA kwa maana uwekezaji una kupata au kukosa kwa hiyo kama ukiwa na mzunguko mzuri wa pesa hata kama utakosa mara moja mara mbili utaweza kujipanga tena kwa mara ya tatu na ya nne. Wengi ya tulioajiriwa au kujiajiri tuko katika hali mbaya kiasi kwamba hatutaki kukosa walau mara moja katika uwekezaji wetu na ndio maana tunashauriwa kutengeneza mzunguko mzuri wa pesa kwanza.

                      DOWNLOAD APP YETU HAPA

No comments:

Post a Comment

Face the challenge