Hawa ni wale ambao kwao ili kuwa na pesa ya pamoja njia nzuri wameona ni kudunduliza/kusevu kidogo kidogo mpaka pale zitakapofikia kiwango walichokipanga. Udundulizaji wa pesa upo wa aina nyingi kuna wale ambao tutaamua kuweka pesa kwenye vibubu vya kawaida au siku hizi vibubu vya kwenye simu, kuweka benki au wengine kwa njia ya VIKOBA. Ubaya wa wengi kama sio wachache lengo la kudunduliza hivi ni kutaka kununua vitu tu vya kawaida vya nyumbani au urembo (kwa wanawake) mfano kununua dera jipya, simu nzuri zaidi n.k. Tunachotakiwa kufahamu ni kwamba si dhambi kudunduliza kama una malengo ya kuwa TAJIRI siku moja, bali ni dhambi kubwa kwa kudunduliza miaka nenda rudi kwa lengo la kununua vitu ambavyo havitakuingizia pesa. Tunachotakiwa ni kudunduliza na kutumia tutakachokipata kwa kununua vitu ambavyo vitatuingizia pesa au kufanya biashara.
Kama na wewe unatunza pesa miaka nenda rudi kwa lengo la kununua kitu fulani ambacho hakitakuingizia pesa...basi nikuamshe tu.....UNAPOTEA. Ila kwa wewe ambae unadunduliza kwa lengo la kufanya biashara au kuna kitu unahisi ukikinunua kitakuingizia pesa basi HONGERA nyingi sana zikufikie popote ulipo ..nikwambie tu kuwa una mawazo ya KITAJIRI.
Watunzaji wa kweli wa pesa wanatunza kwa ajili ya biashara au kwa ajili ya kununua vitu ambavyo vitawaingizia pesa. Ukinunua vitu vya kukuingizia pesa unaweza jikuta umerudisha pesa yako na kitu ulichokinunua bado kipo.
#YouTubeSoon
Tembelea BLOG yetu kutuunga mkono... elimuyautajiri@blogspot.com

No comments:
Post a Comment