elimuyautajiiri.blogspot.com

Tuesday, March 19, 2019

SOMO LA KUMI @elimu_ya_utajiri





Wengi wetu kama sio wote tunawaza kuwa na Uhuru wa pesa siku moja ( kuimilikisha pesa) ila tatizo linakuja pale ambapo tumeamua kufanya fulani na ikaanza kwenye tofauti na tulitegemea, wengi wetu tutaamua kurudi sehemu ambayo tutapata uhakika wa kula na vitu vingine ( kutaka kupokea mshahara kila mwezi) tukisahau kwamba lengo sio kupata uhakika wa kula lengo ni kuja kuitumikisha pesa siku moja. Sasa kama biashara imeenda ndo inaamanisha uachane nayo uanze kuutegemea mshahara pekee?? kwanini usijaribu tena na tena mpaka pale itakapoenda vizuri? au jamani tumejua kuendesha baiskeli ghafla tu bila hata kudondoka dondoka mara mbili mara tatu?? kama tulivyopata mafunzo ya baiskeli ndo mafunzo ya kufanya biashara tuyachukulie hivyo.. Wote sisi ni binadamu ila linapokuja swala la pesa wengi tunaukimbikia ukweli tunaendeshwa na hisia au hofu zetu...ambazo hisia/hofu ndio zinatufanya tuamue kuganda katika eneo fulani(quadrant). Ukitaka kuwa katika eneo lingine lolote  unalolihitaji na kufanikiwa unatakiwa kuwa na maarifa ya yale yanayotolewa darasani. Pia inakupasa kufahamu utofauti mkubwa ambao unawafanya watu kujaribu kuwa katika maeneo tofauti ya yale waliyokuwa nayo sasa. (somo linalofuata). Ukijua utofauti huo utafanya maisha yako yote kuwa rahisi.
Cha kufahamu ni kwamba kila mtu anaweza kubadilika na kuwa katika eneo lolote analolihitaji... ila mabadiliko ya maeneo ya kuzalisha pesa ni tofauti na badiliko la kazi yaani kuamua kuacha kazi hii na kwenda kufanya kazi nyingine au kubadilisha taaluma ( mfano kutoka uhasibu kwenda kuwa mwalimu). Kubadilisha eneo (quadrant) kunahusisha na kubadilisha mtazamo  yaani jinsi unavyofikiri na jinsi unavyoifikiria dunia ya sasa. Badiliko la eneo ni rahisi kwa baadhi ya watu na ni ngumu kweli kwa baadhi ya watu wengine. Hii hutokana na kwamba kuna watu wako tayari kukubaliana na mabadiliko kuna wengine wao wako tayari kupingana na mabadiliko huku wakitetea mitazamo yao iliyopitwa na wakati. Badiliko la eneo ni suala ambalo ni la kujifunza maisha yako yote kwa kupata maarifa na uzoefu wa kila hatua unayokwenda sio jambo la siku moja au mbili. Unajifunza kutokana na mabadiliko ya wakati na dunia hii na kujua kutumia fursa.

No comments:

Post a Comment

Face the challenge