elimuyautajiiri.blogspot.com

Tuesday, March 19, 2019

SOMO LA KUMI NA TISA @elimu_ya_utajiri




Baada ya kuona hali za wastaafu wengi wa serikalini na wengine baada ya kuwaona watu wengi waliojiajiri wakipata tabu sana pale wanapopata ugonjwa au wanavyoendesha maisha yao ya kila siku bila hata kupumzika, sasa tunajikuta tunalazimika kuwekeza bila ya kuwa na ELIMU YA UWEKEZAJI. 
Na wengi waliokuwa wanaogopa kupoteza pesa zao (RISK) kipindi wanafanya kazi wanalazimika kufanya kile kile walichokiogopa wakistaafu....Hivi hatuwashuhudii wafanyakazi wengi wakihangaika kutafuta miradi ya kuwekeza wakishastaafu? Kama kweli tunaogopa kupoteza pesa kwa nini sasa tuko tayari kuwekeza ukifikia muda wa kustaafu? Naweza sema...Mshahara wa kila mwezi kwa upande wa wafanyakazi na afya njema na umri kwa upande wa watu waliojiajiri vinatudanganya.... TUAMKE. 
Na kama hautafahamu leo haya ninayokwambia basi subiri mpaka pale utakapostaafu au umri utakapoenda uje uieleze ukweli dunia wewe mwenyewe. 
Ili uwe mwekezaji lazima uwe mwekezaji......hii inamaanisha lazima uwe na elimu ya uwekezaji ili uweze kujiita wewe ni MWEKEZAJI. Tatizo wengi ya waajiriwa na waliojiajiri asili yetu ni kutaka uhakika wa maisha (mshahara) na  ndio maana tunatafuta kazi au kuanzisha biashara  ndogondogo tunazoweza kuzimudu (waliojiajiri). Kwa kuwa wengi tumeshazoea uhakika wa maisha.....basi hata tunapotaka kuwekeza tunakuja kwa lengo la kutafuta uhakika huo huo, kumbe sio kweli kuwekeza ni sehemu ambayo inahusisha sana HOFU YA KUPOTEZA PESA(RISK) kuliko ule uhakika ambao wengi wetu tunaufuata. Kwa kufuata huu uhakika basi hili ni moja ya jambo ambalo wengi tunalifanya huku hatujui kama tunakosea:

KUWEKEZA KATIKA MAENEO MENGI
Wengi tunaamua kuwekeza maeneo mengi ili kuhakikisha kwamba hatupotezi pesa zetu.....yaani mtu atafungua duka la bidhaa ya chakula, atanunua boda boda,atauza nguo n.k.... yaani ili mradi tu ahakikishe huku kukienda vibaya basi huku kunaenda vizuri. Uwekezaji haushauri hivyo bali unashauri tafuta sehemu chache za kuwekeza halafu elekeza nguvu zako na akili zako huko na ukabiliane na kila hali. Wawekezaji waliofanikiwa au MATAJIRI hawafanyi hivyo bali wanaweka nguvu sehemu chache. 
KIKUBWA KATIKA KUWEKEZA INABIDI TUSIENDE NA MAWAZO YA KUOGOPA KUPOTEZA PESA.
#WhatsappNoSoon

No comments:

Post a Comment

Face the challenge